Barua Pepe | Facebook | Instagram | Twitter |

Elimu ya Afya kwa Umma

ELIMU YA MAGONJWA

Kujikinga na kujilinda dhidi ya magonjwa ni  muhimu  kwa ajili ya afya zetu. Zipo njia mbalimbali za kujikinga zidi ya magonjwa kwa njia ya maji, chakula, wanyama, wadudu na watu.

MAJI

  • Vimelea wengi wanaweza “kuingia” moja kwa moja katika mwili wako kupitia maji machafu.

Namna ya kujikinga

  •  Njia bora zaidi ya kujikinga ni kutumia maji yaliyo safi na salama.Ukijua kwamba maji unayotumia yana vimelea au si salama, unapaswa kuyatibu. Hifadhi maji ya kunywa kwenye chombo kilichofunikwa, na uchote kwa kutumia chombo safi. Usitumbukize mikono yako kwenye chombo chenye maji safi. Inapowezekana, ishi mahali au katika nyumba zenye mfumo mzuri wa kuondoa taka ili kuepusha kuchafua vyanzo vya maji.


CHAKULA

  • Vimelea hatari vinaweza kuwepo au kuingia kwenye chakula chako.

Namna ya kujikinga

  • Chakula au matunda yenye bakteria, huenda yakaonekana kuwa salama na mazuri. Kwa hiyo uwe na kawaida ya kuosha vizuri matunda na mboga kabla ya kuzitumia. Hakikisha kwamba mikono yako, vyombo vya chakula, na mazingira ya jikoni, ni safi kabla ya kuanza kutayarisha na kuandaa chakula. Baadhi ya vyakula vinahitaji kupikwa kwa joto la kiwango fulani ili kuua vimelea hatari.


WADUDU

  • Baadhi ya wadudu wanaweza kukuambukiza vimelea hatari vilivyo katika miili yao.

Namna ya kujikinga

  • Dhibiti maambukizi yanayosababishwa na wadudu kwa kukaa ndani ya nyumba au kwa kuvaa nguo zinazofunika mwili kama vile sweta na suruali. Lala ndani ya chandarua chenye dawa, na upake dawa za kujikinga na wadudu. Ondoa vyombo vyenye maji yaliyotuama, mahali ambako mbu wanaweza kuzaliana. 


WATU

  •  Baadhi ya vimelea vinaweza kuingia mwilini mwako kupitia umajimaji unaotoka baada ya mtu kukohoa au kupiga chafya. Pia, vimelea vinaweza kuenea kupitia kugusana kimwili kwa kukumbatiana na kusalimiana kwa mikono. Vimelea kutoka kwa watu wengine vinaweza pia kupatikana kwenye vitasa vya milango, vishikio vya ngazi, simu, rimoti, skrini za kompyuta na kibodi.

Namna ya kujikinga

  •  Usitumie vifaa kama vile, wembe, mswaki, au taulo na watu wengine. Epuka kugusa umajimaji kutoka kwa wanyama au watu wengine, kutia ndani damu na vitu vinavyotokana na damu. Ni muhimu sana kunawa mikono yako vizuri na kwa ukawaida. Hiyo ni moja ya njia bora za kuepuka kueneza magonjwa.
read more
ELIMU YA LISHE

Lishe bora maana yake ni kula chakula cha kutosha na chakula chenye virutubisho vyote muhimu. Lishe bora  husaidia mwili kukua vyema, kuujenga mwili lakini pia huimarisha kinga ya mwili ili kuweza  kupigana na magonjwa. Ili lishe iwe bora ni muhimu iwe na mchanganyiko wa vyakula mbalimbali kama vile protini, wanga, fati, mbogamboga, madini, matunda na maji kwa wingi .

read more
ELIMU YA USAFI
  • Kama tunavyojua usafi wa mazingira na mwili  ni njia ya kuendeleza afya kwa kuzuia mawasiliano ya binadamu na athari za taka.  Usafi kama njia ya kuzuia maradhi inaweza kutumika kwa usahihi  kabisa ili kuzuia maradhi na milipuko ya magonjwa mbalimbali hivyo ni muhimu kufanya usafi katika mazingira yanayokuzunguka lakini pia kunawa mikono  kwa maji safi na sabuni baada ya kutoka chooni.
  • Upungufu wa usafi wa mazingira ni sababu kuu ya maradhi duniani kote. Uboreshaji wa usafi wa  mazingira una manufaa makubwa kwa afya ya wote katika kaya na katika jamii. Usafi wa mazingira unahusu pia udumishaji wa ratiba ya usafi, kwa njia ya huduma kama vile ukusanyaji wa taka na maji machafu.
read more
CORONA (COVID-19)
ELIMU YA VIRUSI VYA EBOLA

12

3

4

5

6

read more
UGONJWA WA MARBURG

Ugonjwa wa Marburg ni nini?

Kulingana na Umoja wa Mataifa, virusi vya Marburg, ambavyo ni sawa na virusi hatari vya Ebola, viligunduliwa kwa mara ya kwanza baada ya watu 31 kuambukizwa, saba kati yao walikufa, mnamo 1967 huko Marburg na Frankfurt. Ujerumani na Belgrade huko Serbia.

Dalili za ugonjwa huo ni pamoja na kikohozi, maumivu ya viungo, kuhara na kutapika, na mara nyingi hata upungufu wa damu katika mwili.

Mlipuko huo ulitokana na tumbili wa Kiafrika walioagizwa kutoka Uganda. Lakini virusi hivyo vimehusishwa na wanyama wengine tangu wakati huo.

Na miongoni mwa wanadamu, huenezwa zaidi na watu ambao wamekaa kwa muda mrefu katika mapango na migodi iliyo na popo.

Unaanza ghafla na:

  • Homa
  • Kuumwa vibaya na kichwa
  • Kuumwa na misuli

Hii mara nyingi siku tatu hufuatwa na:

  • Kuharisha
  • Kuumwa na tumbo
  • Kichefuchefu
  • Kutapika

Ugonjwa wa Marburg unaenezwa kwa

Popo wa matunda aina ya rousette wa Misri mara nyingi huwa na virusi. Nyani wa kijani kibichi na nguruwe wanaweza pia kubeba.

Miongoni mwa wanadamu, huenea kupitia maji ya mwili na malazi yaliyochafuliwa nao.

Na hata watu wakipona, damu au shahawa zao, kwa mfano, zinaweza kuwaambukiza wengine kwa miezi mingi baadaye.

Je, inaweza kutibiwaje?

Hakuna chanjo maalum au matibabu ya virusi.

Vinawezaje kudhibitiwa?

Watu barani Afrika wanapaswa kuepuka kula au kushika nyama ya porini.

Na wale wanaozika watu ambao wamekufa kutokana na virusi wanapaswa kuepuka kugusa mwili.

read more
HOMA YA INI

Kitaalam, ugonjwa huu wa ini   husababishwa na virusi vya Hepatitis B(HBV)ambayo vinathiri  mifumo wa utoaji wa sumu katika  mwilini wa binadamu. Inaaminika kwamba robo tatu ya watu ulimwenguni  wameathiriwa na vinyemelea vya   homa ya ini na wengine milioni 350 wameathirika moja kwa moja. 


 SABABU ZINAZOPELEKEA KUPATA HOMA YA INI

  • Ulevi wa kupindukia hasa kwa wale wanaotumia mapombe ya kienyeji ambayo hayana kiwango.
  • Sumu inapoingia mwilini ( chakula, chenye sumu).
  • Kuambukizwa kwa kufanya tendo la ndoa kwa kushikana na majimaji ya mwili wa mtu aliyeathirika ikiwa ni pamoja na damu, mate, machozi na mkojo.

DALILI ZA HOMA YA INI.

Ugonjwa ini huchukua muda mrefu  kuonekana na zikionekana mgonjwa anakuwa tayari amekwisha athirika sana.

  • Kuumwa na kichwa bila mpangilio.
  • Kusikia kichefu chefu
  • Kukosa hamu ya kula na kupungua uzito
  • Maumivu makali ya tumbo upande wa ini
  • Macho na ngozi kubadilika na kuwa rangi ya manjano ya njano
  • Choo kibwa na na kidogo kuwa  na rangi  ya manjano.
  • Kuvimba tumbo katika hatua za mwisho

Kwa maelezo zaidi tembelea katika Hospitali yetu ikiwa una dalili kadhaa.

read more