Barua Pepe | Facebook | Instagram | Twitter |

HOMA YA INI

Posted on: October 17th, 2019

Kitaalam, ugonjwa huu wa ini   husababishwa na virusi vya Hepatitis B(HBV)ambayo vinathiri  mifumo wa utoaji wa sumu katika  mwilini wa binadamu. Inaaminika kwamba robo tatu ya watu ulimwenguni  wameathiriwa na vinyemelea vya  homa ya ini na wengine milioni 350 wameathirika moja kwa moja. 

 SABABU ZINAZOPELEKEA KUPATA HOMA YA INI

  • Ulevi wa kupindukia hasa kwa wale wanaotumia mapombe ya kienyeji ambayo hayana kiwango.
  • Sumu inapoingia mwilini ( chakula, chenye sumu).
  • Kuambukizwa kwa kufanya tendo la ndoa kwa kushikana na majimaji ya mwili wa mtu aliyeathirika ikiwa ni pamoja na damu, mate, machozi na mkojo.

DALILI ZA HOMA YA INI.

Ugonjwa ini huchukua muda mrefu  kuonekana na zikionekana mgonjwa anakuwa tayari amekwisha athirika sana.

  • Kuumwa na kichwa bila mpangilio.
  • Kusikia kichefu chefu
  • Kukosa hamu ya kula na kupungua uzito
  • Maumivu makali ya tumbo upande wa ini
  • Macho na ngozi kubadilika na kuwa rangi ya manjano ya njano
  • Choo kibwa na na kidogo kuwa  na rangi  ya manjano.
  • Kuvimba tumbo katika hatua za mwisho

Kwa maelezo zaidi tembelea katika Hospitali yetu ikiwa una dalili kadhaa.